Image and video hosting by TinyPic Image and video hosting by TinyPic
 

Unknown Unknown Author
Title: EL DERBI MADRILEÑO: NGOMA NGUMU, ILA REAL WAPAA NAFASI YA PILI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
El Derbi Madrileno, Mechi ya Mahasimu wa Jiji la Madrid huko Spain, Atletico Madrid na Real Madrid, iliyochezwa Vicente Calderon imem...
El Derbi Madrileno, Mechi ya Mahasimu wa Jiji la Madrid huko Spain, Atletico Madrid na Real Madrid, iliyochezwa Vicente Calderon imemalizika kwa Sare ya 1-1.
Real walitangulia kufunga katika Dakika ya 9 baada ya Krosi ya Carvajal kuunganishwa kwa Kichwa na Karim Benzema na kumwacha Kipa wa Atletico Oblak akidaka hewa.
Katika Dakika ya 20 Atletico walipewa Penati kufuatia rafu ya Ramos kwa Tiago na Griezmann kupiga Penati hiyo ambayo Kipa wa Real Navas aliikoa.
Hadi Haftaimu, Atletico 0 Real 1.
Bao la kusawazisha la Atletico lilifungwa Dakika ya 84 na Luciano Vietto, Mchezaji alietokea Benchi Dakika ya 58 kumbadili Angel Correa.
Matokeo haya yamewapaisha Real na kukamata Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 1 nyuma ya Vinara Villareal.
VIKOSI:
Atletico Madrid: Oblak; Juanfran, Gimenez, Godin, Filipe; Tiago, Gabi, Oliver; Griezmann, Torres, Correa.
Real Madrid: Navas; Carvajal, Varane, Sergio Ramos, Marcelo; Casemiro, Kroos, Modric; Isco, Ronaldo, Benzema.

LA LIGA MATOKEO:
Ijumaa Oktoba 2
Celta de Vigo 0 Getafe CF 0
Jumamosi Oktoba 3
Sevilla FC 2 FC Barcelona 1
Granada CF 1 Deportivo La Coruna 1
RCD Espanyol 1 Sporting Gijon 2
Las Palmas 0 SD Eibar 2
Malaga CF 3 Real Sociedad 1
Jumapili Oktoba 4
Rayo Vallecano 0 Real Betis 2
Athletic de Bilbao 3 Valencia C.F 1
Levante 1 Villarreal CF 0

Atletico de Madrid 1 Real Madrid CF 1

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top