Image and video hosting by TinyPic Image and video hosting by TinyPic
 

Unknown Unknown Author
Title: MAN CITY WATATU WAENDA MKOPO SIKU YA MWISHO YA USAJILI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Bado masaa machache tu kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya,vilabu  mbalimbali barani humo vimeendelea kupigana vikumbo vi kiwania s...

Bado masaa machache tu kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya,vilabu  mbalimbali barani humo vimeendelea kupigana vikumbo vikiwania saini za wachezaji kutoka klabu fulani.

Mpaka sasa klabu ya Manchester City imefanikiwa kuwatoa wachezaji wake watatu kwenda kwa mkopo katika klabu tofauti tofauti ambao walikuwa hawapo katika mipango ya Pep Guardiola.

Wachezaji waliotolewa na klabu ya Manchester City ni hawa:

• WILFRED BONY

Muivory cost huyu amefanikiwa kupata timu ambayo itamwezesha kuendelea kukipiga katika ligi ya England,Wilfred Bony amesajiliwa kwa mkopo wa muda mrefu na klabu ya Stoke City.

•SAMIR NASRI

Klabu ya nchini Hispania Sevilla Fc imefanikiwa kumsajili mchezaji Samir Nasri kwa mkataba wa mkopo wa muda mrefu akitokea Manchester City.

•ELIAQUIM MANGALA

Eliaquim Mangala amefanikiwa kupata timu na hii kutokana na klabu ya Valencia kumtoa mchezaji wao Mustafi aliye jiunga na Arsenal, Mangala amejiunga na Valencia kwa mkataba wa mkopo wa muda mrefu akitokea Manchester City.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top