Ligi kuu Tanzania bara imeendelea jana kwa michezo miwili ya kati ya Azam vs Mtibwa mjini morogoro huku Yanga vs mwadui uwanja wa Taifa
Yanga walikuwa wakwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Simon Msuva dakika ya tatu kipindi cha kwanza kabla ya Kelvin Sabath kuisawazishia Mwadui FC dakika 10 baadaye
Yanga walikuwa wakwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Simon Msuva dakika ya tatu kipindi cha kwanza kabla ya Kelvin Sabath kuisawazishia Mwadui FC dakika 10 baadaye
Mpaka mapumziko Yanga 1-1 Mwadui moja Huku mchezo ukionekana kuwa wakupaniana, kipindi cha pili kilioanza kwa kasi kila timu ikisaka bao Yanga walipata goili la pili na la ushindi kupitia kiungo wake haruna niyonzima katika dakika za lala salama na kuwafanya Yanga kutoka na ushindi wa bao 2-1
Mkoani Morogoro Azam FC ilichomoza na ushindi wa bao 1-0 wakiwafunga wenyeji Mtibwa sugar mchezo uliopigwa katika dimba la Manungu Complex
Ushindi wa Yanga unaifanya kufikisha jumla ya pointi 56 pointi moja nyuma ya vinara wa ligi hiyo Simba SC lakini Simba ikiwa mbele kwa mchezo mmoja.



Post a Comment