Kiungo mpya wa Manchester United Paul Pogba hatacheza mechi ya ufunguzi wa msimu mpya wa ligi kuu nchini Uingereza ambapo mashetani hao watacheza dhidi ya Bournemouth ugenini.
Pogba,23, hatacheza mechi hiyo kwa sababu atakuwa akitumikia adhabu ya kifungo cha mechi moja kufuatia kupata kadi 2 za njano katika mechi 2 za mwisho za Coppa Italia msimu ulioisha.
.
"Amepata kadi 2 za njano katika mechi 2 za mwisho za Coppa italia ambapo adhabu yake ni kufungiwa mechi moja" wameeleza FA
Sheria za chama cha soka cha Uingereza FA zinasema kuwa kwa mchezaji yoyote ambaye atakuwa na adhabu kutoka ligi nyingine ataibeba adhabu yake endapo atahamia ligi ya Uingereza.
Post a Comment