Image and video hosting by TinyPic Image and video hosting by TinyPic
 

Unknown Unknown Author
Title: RAIS MALINZI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUNISHI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Rais wa TFF, Jamal Malinzi amepokea kwa masikitiko kifo cha Boniventur Munishi ambaye ni Baba mzazi wa Golikipa wa Young Africans na timu ya...

Rais wa TFF, Jamal Malinzi amepokea kwa masikitiko kifo cha Boniventur Munishi ambaye ni Baba mzazi wa Golikipa wa Young Africans na timu ya Tanzania 'Taifa Stars' , Deogratius Munishi.
Kifo cha Munishi kilitokea jana Agosti 28, 2016  jijini Dar es Salaam.
Kutokana na kifo hicho, Rais Malinzi ametuma salaam za rambirambi kwa familia na ukoo wote wa Munishi akiwasii kuwa watulivu wakati huu mgumu kwao kwa kumpoteza mpendwa wao.
Mungu aipumzishe Roho ya Marehemu mahali pema peponi.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

IMETOLEWA NA TFF

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top