Image and video hosting by TinyPic Image and video hosting by TinyPic
 

Unknown Unknown Author
Title: MAN UNITED WAWEKA REKODI YA MAPATO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya Manchester United imetangaza kuingiza mapato ya Pauni milion 515.3 kwa mwaka wa fedha 2016 na kuwa klabu ya kwanza ya Uingereza kui...

Klabu ya Manchester United imetangaza kuingiza mapato ya Pauni milion 515.3 kwa mwaka wa fedha 2016 na kuwa klabu ya kwanza ya Uingereza kuingiza kiasi hicho.
Katika mwaka huo timu hiyo ilishinda kombe la FA,ilisaini mikataba 14 ya wadhamini na biashara,mapato ya mechi,mapato ya Televisheni yameongezeka
Sasa inakadiriwa mapato hayo kufikia pauni milioni 540 kwa mwaka 2017 licha ya kuwa hawapo katika michuano ya klabu bingwa ulaya.
Man United imekuwa timu ya kwanza ya Uingereza kufikia mapato ya nusu bilioni ndani ya mwaka mmoja, wakiweka rekodi ya faida pauni milioni 68.
Mabingwa wa La Liga Barcelona mapema mwaka huu walitangaza kuingia mapato ya pauni milioni 571, hivyo Man United wamekuwa wapili kwa mapato Barca wakiwa wa kwanza.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top