Image and video hosting by TinyPic Image and video hosting by TinyPic
 

Unknown Unknown Author
Title: SAM ALLARDYCE MATATANI UINGEREZA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kibarua cha Allardyce England matatani, akumbwa na tuhuma kubwa za rushwa Meneja wa Timu ya Taifa ya England Sam Allardyce anaweza kupoteza...

Kibarua cha Allardyce England matatani, akumbwa na tuhuma kubwa za rushwa
Meneja wa Timu ya Taifa ya England Sam Allardyce anaweza kupoteza kibarua chake mbele ya FA baada ya kuiwezezesha timu hiyo kucheza mchezo mmoja tu kufuatia tuhuma za kutumia vibaya kiti chake kujipatia kiasi cha euro 400,000 kwa nja isiyo halali.

Allardyce anatuhumiwa kutumia nafasi yake kumsaidia moja ya wafanyabiashara wakubwa kutumia njia za panya na kuvunja sheria za uhamisho wa wachezaji za FA.

FA imethibitisha kwamba imepata tuhuma hizo na wanasubiri taarifa kwa undani kabla ya kuchukua hatua zinazostahili.

Mzungumzaji wa FA amesema: “Tunawaomba Daily Telegraph kutupatia ukweli wote juu ya hili suala ili tuweze kulifanyia kazi kwa usahihi .” Gazeti la Telegraph linadia kwamba Allardyce alitumia nafasi yake ya umeneja wa England kuingia makubaliano ya kijipatia kiasi cha euro 400,000 ili kumshauri mfanyabishara mmoja kupita mlango wa nyuma na kuvunja sheria za usajili za wachezaji za FA.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top