Timu ya taifa ya Wanawake ya Tanzania "Tanzania Queens" leo hii wamefuzu hatua ya Nusu fainali katika mchezo waliocheza na Ethiopia.
Katika mchezo uliopigwa mjini Kampala dhidi ya Ethiopia mchezo huu ulimalizika sare ya 0-0 na timu hizi zilionekana zote kulingana Pointi 4 na kulingana utofauti wa magoli yaani Goal Deference 1
.Kwa kutokana na usawa huu katika kila kitu kulingana na ndipo mwamuzi akatumia maamuzi yake kwa kuumalizisha mchezo huu kwa kurusha shilingi ili apatikane mshindi wa kundi. Na ndipo Tanzania Queens waliweza kufuzu katika hatua hii ya urushaji shilingi kwa kuangukia upande wao.
Hivyo basi Tanzania Queens watacheza Nusu Fainali dhidi ya Uganda siku ya Jumapili.


Post a Comment