NA:Fredy Reuben
Kiungo wa club ya Manchester United Ander Herrera amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Spain kwa Mara ya kwanza chini ya mwalimu Julen Lopetegui
Herrera (27)amekuwa na msimu mzuri tangu mwalimu JOSEE MOURINHO alivoanza kumpa nafasi ya kucheza na Paul pogba katika sehemu ya kiungo! Baada ya fellain kuonekana kutokufanya vizur pindi anapocheza na pogba!
Ander Herrera kwa Mara ya kwanza anaitwa kwenye timu ya Taifa ya wakubwa baada ya kucheza kwenye ngazi za U20,U21, U23, !
Herrera ameitwa kwenda kuziba nafasi za Thiago Alcantara na Saul Niguez ambao wote hawa wanasumbuliwa na majeruhi!
Spain wanajiandaa na michezo ya kufuzu kuelekea Fainali za kombe la Dunia 2018 zitakazo fanyika nchini Urusi ambapo mchezo wa kwanza watacheza na Italy siku ya Alhamisi kabla ya kwenda kuwavaa Albania siku chache mbeleni!


Post a Comment