Real Madrid sasa wataweza kusajili wachezaji katika kipindi cha kiangazi mwaka 2017 baada ya kupunguziwa adhabu na mahakama ya usuluhishi ya michezo.
Mapema mwaka huu FIFA ilitangaza kuzipiga marufuku klabu za Real Madrid na Atletico Madrid kufanya usajili kwa vipindi viwili kufuatia kuvunja taratibu na sheria za usajili wa wachezaji chini ya miaka 18 kutoka nje.
Adhabu hiyo ilikuwa ni ya vipindi viwili vya usajili vya mwaka 2017, lakini baada ya mabingwa hao wa Ulaya na dunia kukata rufaa, wamepunguziwa huku mahasimu wao Atletico Madrid wakiwa bado hawajapewa neno lolote kutoka katika mahakama hiyo.
Post a Comment