Kikosi cha Mabingwa wa tetezi YangaSC ilifika salama salmini mkoani Songea jana Jioni majira ya saa moja usiku.
Yanga Sc walipata mapokezi makubwa sana toka kwa wana Yanga wa mkoa wa songea kiukweli yamemgusa mwalimu mkuu nakujikuta akishindwa ficha hisia zake juu ya mashabiki hao.
Akiongea na Balozisportsite mara baada ya kufika mkoani songea haya ndio yalikuwa maneno ya mwalimu mkuu George Lwandamila.
"Kwakweli ni kitu kipya sana kwenye maisha yangu ya mpira kwani hawa watu wanaonyesha upendo wa dhati kwa timu yao kuanzia tunaanza safari kila tulipopita tulipata mapokezi ya hali ya juu toka kwa mashabiki wa Yanga kweli wanaopenda sana timu yao sasa hii inazidi nipa changamoto kubwa na kupambana mimi na vijana wangu kuwapa furaha mashabiki hawa kwa kuchukua point tatu hapo kesho dhidi ya maji maji."
Pia aliongeza kwa kusema
"asanteni sana wana Yanga kote tulipopita mpaka kufika hapa Songea nimefurai sana jinsi mnavyoipenda timu yenu na naomba muendelee kuwa na moyo huo huo kwa timi yenu"
Post a Comment